Publicidade

Salmos 112

Baraka za mwenye haki

1 Haleluya.

Heri mtu yule amchaye BWANA,

Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazawa wake watakuwa hodari duniani;

Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.

3 Mit 3:16;15:6;Isa 33:6;Mt 6:33;2 Kor 6:10 Nyumbani mwake mna utajiri na mali,

Na haki yake yadumu milele.

4 Nuru huwaangaza wenye adili gizani;

Ana fadhili na huruma na haki.

5 Lk 6:35 Heri atendaye fadhili na kukopesha;

Atengenezaye mambo yake kwa haki.

6 Kwa maana hataondoshwa kamwe;

Mwenye haki atakumbukwa milele.

7 Hataogopa habari mbaya;

Moyo wake u imara ukimtumainia BWANA.

8 Moyo wake umethibitika hataogopa,

Hata awaone watesi wake wameshindwa.

9 Lk 11:41;Rum 12:13;Mdo 4:35;20:35;2 Kor 8:9;9:9;1 Tim 6:18 Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini,

Haki yake yakaa milele,

Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.

10 Lk 13:28 Asiye haki ataona na kusikitika,

Atasaga meno yake na kuondoka,

Matumaini ya wasio haki hupotea.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-