Palavras de consolo
A Bíblia é repleta de palavras de consolo para os aflitos. Deus está perto dos que sofrem e promete enxugar toda lágrima, renovar a esperança e restaurar o coração partido.
Deus está conosco
O Senhor é refúgio e fortaleza. Mesmo no vale da sombra da morte, não precisamos temer — Ele está ao nosso lado para nos consolar.
Hata nikipita katikati
ya bonde la uvuli wa mauti,
sitaogopa mabaya,
kwa maana wewe upo pamoja nami;
fimbo yako na mkongojo wako
vyanifariji.
Sala ya kusifu
Mwenyezi Mungu ni nuru yangu na wokovu wangu,
nimwogope nani?
Mwenyezi Mungu ni ngome ya uzima wangu,
nimhofu nani?
Mwenyezi Mungu ni kimbilio la wanaodhulumiwa,
ni ngome imara wakati wa shida.
Jambo moja ninamwomba Mwenyezi Mungu,
hili ndilo ninalolitafuta:
niweze kukaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu
siku zote za maisha yangu,
niutazame uzuri wa Mwenyezi Mungu
na kumtafuta hekaluni mwake.
Kwa kuwa siku ya shida,
atanihifadhi salama katika maskani yake,
atanificha uvulini mwa hema lake,
na kuniweka juu kwenye mwamba.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mungu Mwenyezi,
tegemeo langu tangu ujana wangu.
Consolação e esperança
Deus consola os humildes e exalta os abatidos. Ele nunca nos desamparará.
Mwenyezi Mungu mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike."
Msiwaogope, Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atapigana kwa ajili yenu."
Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wako, atakuwa pamoja nawe popote utakapoenda."
Huwainua juu wanyonge,
nao wale wanaoomboleza
huinuliwa wakawa salama.
Bwana wetu Isa Al-Masihi mwenyewe na Mungu, Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema,
Descanso e renovação
Bem-aventurados os que choram, pois serão consolados. A Bíblia nos convida a descansar nos braços do Pai e encontrar paz para a alma.
Heri wale wanaohuzunika,
maana hao watafarijiwa.
Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake. Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye anajishughulisha sana na mambo yenu.
Nipe ishara ya wema wako,
ili adui zangu waione nao waaibishwe,
kwa kuwa wewe, Ee Mwenyezi Mungu,
umenisaidia na kunifariji.
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu,
sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
unapolala, hutaogopa;
unapolala, usingizi wako utakuwa mtamu.
Kila jambo lina wakati wake
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo,
nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,
wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa yaliyopandwa,
wakati wa kuua na wakati wa kuponya,
wakati wa kubomoa,
na wakati wa kujenga,
wakati wa kulia na wakati wa kucheka,
wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,
wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe,
wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza,
wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,
wakati wa kurarua na wakati wa kushona,
wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,
wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia,
wakati wa vita na wakati wa amani.