28" ‘Msichanje chale miili yenu kwa ajili ya mfu, wala msijichore alama juu ya miili yenu. Mimi ndimi Bwana.
36Tumia mizani halali, mawe ya kupimia uzito halali, efa19:36 Efa kilikuwa kipimo cha vitu vikavu. halali, na hini19:36 Hini kilikuwa kipimo cha vitu vimiminika. halali. Mimi ndimi Bwana Mungu wako, ambaye alikutoa katika nchi ya Misri.
5alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
8Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
15Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani.Neema iwe nanyi nyote. Amen.
7Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
15Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
16ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
14Lakini, ninakubali kwamba mimi namwabudu Mungu wa baba zetu, mfuasi wa Njia, ile ambayo wao wanaiita dhehebu. Ninaamini kila kitu kinachokubaliana na Sheria na kile kilichoandikwa katika Manabii,
15nami ninalo tumaini kwa Mungu, ambalo hata wao wenyewe wanalikubali kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, kwa wenye haki na wasio na haki.
16Kwa hiyo ninajitahidi siku zote kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
1Roho wa Bwana Mwenyezi yu juu yangu,kwa sababu Bwana amenitia mafutakuwahubiria maskini habari njema.Amenituma kuwaganga waliovunjika moyo,kuwatangazia mateka uhuru wao,na hao waliofungwahabari za kufunguliwa kwao;
6Nanyi mtaitwa makuhani wa Bwana,mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.Mtakula utajiri wa mataifa,nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
10Ninafurahia sana katika Bwana,nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu.Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu,na kunipamba kwa joho la haki,kama vile bwana arusi apambavyokichwa chake kama kuhani,na kama bibi arusi ajipambavyokwa vito vyake vya thamani.
9Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu,
12mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote,
4Je, wewe hujaniita hivi punde tu:‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
13Ungama dhambi zako tu:kwamba umemwasi Bwana Mungu wako,umetapanya wema wako kwa miungu ya kigenichini ya kila mti unaotanda,nawe hukunitii mimi,’ "asema Bwana.
25Sisi na tulale chini katika aibu yetu,na fedheha yetu itufunike.Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu,sisi na mababa zetu;tangu ujana wetu hadi leohatukumtii Bwana Mungu wetu."
9Kuhusu manabii:Moyo wangu umevunjika ndani yangu;mifupa yangu yote inatetemeka.Nimekuwa kama mtu aliyelewa,kama mtu aliyelemewa na divai,kwa sababu ya Bwanana maneno yake matakatifu.
25"Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
26Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
1Palikuwa na mtu aliyeitwa Mika ambaye aliishi katika vilima vya Efraimu.
4Hivyo akamrudishia mama yake ile fedha, naye mama yake akachukua shekeli mia mbili17:4 Shekeli 200 za fedha ni sawa na kilo 2.3 za fedha. za hiyo fedha na kumpa mfua fedha, ambaye aliifanyiza kinyago na sanamu. Navyo vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika.
8Huyu kijana akatoka katika mji huo wa Bethlehemu ya Yuda na kutafuta mahali pengine ambapo angeweza kuishi. Alipokuwa akisafiri, akafika nyumbani kwa Mika katika vilima vya Efraimu.
2"Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi:" ‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda.