Publicidade

Salmos 23

Bwana Mchungaji Wetu
Zaburi ya Daudi.

1 Bwana ndiye mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2 Hunilaza katika malisho

ya majani mabichi,

kando ya maji matulivu huniongoza,

3 hunihuisha nafsi yangu.

Huniongoza katika njia za haki

kwa ajili ya jina lake.

4 Hata kama nikipita katikati

ya bonde la uvuli wa mauti,

sitaogopa mabaya,

kwa maana wewe upo pamoja nami;

fimbo yako na mkongojo wako

vyanifariji.

5 Waandaa meza mbele yangu

machoni pa adui zangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na upendo vitanifuata

siku zote za maisha yangu,

nami nitakaa nyumbani mwa Bwana

milele.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-