Publicidade

Salmos 8

Utukufu Wa Mungu Na Heshima Ya Mwanadamu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Daudi.

1 Ee Bwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Umeuweka utukufu wako

juu ya mbingu.

2 Midomoni mwa watoto wachanga na wanyonyao

umeamuru sifa,

kwa sababu ya watesi wako,

kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3 Nikiziangalia mbingu zako,

kazi ya vidole vyako,

mwezi na nyota,

ulizoziratibisha,

4 mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,

binadamu ni nani hata unamjali?

5 Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni,

ukamvika taji ya utukufu na heshima.

6 Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;

umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.

7 Mifugo na makundi yote pia,

naam, na wanyama wa kondeni,

8 ndege wa angani na samaki wa baharini,

naam, kila kiogeleacho katika njia za bahari.

9 Ee Bwana, Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-