Publicidade

Salmos 146

Kumsifu Mungu Mwokozi

1 Msifuni Bwana! kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,

2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote;

nitamwimbia Mungu wangu sifa

wakati wote niishipo.

3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu,

kwa wanadamu ambao hufa,

ambao hawawezi kuokoa.

4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini,

siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.

5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,

ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,

6 Muumba wa mbingu na nchi,

na bahari na vyote vilivyomo ndani yake:

Bwana anayedumu kuwa mwaminifu

milele na milele.

7 Naye huwapatia haki walioonewa

na kuwapa wenye njaa chakula.

Bwana huwaweka wafungwa huru,

8 Bwana huwafumbua vipofu macho,

Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao,

Bwana huwapenda wenye haki.

9 Bwana huwalinda wageni

na kuwategemeza yatima na wajane,

lakini hupinga njia za waovu.

10 Bwana atamiliki milele,

Mungu wako, ee Sayuni,

kwa vizazi vyote.

Msifuni Bwana.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-