Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 70

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.

1 Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

Ee Bwana, njoo hima unisaidie.

2 Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

3 Wale waniambiao, "Aha! Aha!"

warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4 Lakini wote wakutafutao

washangilie na kukufurahia,

wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,

"Mungu na atukuzwe!"

5 Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

Ee Bwana, usikawie.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também