Publicidade

Salmos 82

Maombi Kwa Ajili Ya Kutaka Haki
Zaburi ya Asafu.

1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,

anatoa hukumu miongoni mwa "miungu":

2 "Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki

na kuonyesha upendeleo kwa waovu?

3 Teteeni wanyonge na yatima,

tunzeni haki za maskini na walioonewa.

4 Mwokoeni mnyonge na mhitaji,

wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.

5 "Hawajui lolote, hawaelewi lolote.

Wanatembea gizani;

misingi yote ya dunia imetikisika.

6 "Nilisema, ‘Ninyi ni "miungu";

ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’

7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;

mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote."

8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,

kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-