Publicidade

Salmos 15

Kitu Mungu Anachotaka
Zaburi ya Daudi.

1 Bwana, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2 Ni yule aendaye pasipo mawaa,

atendaye yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake,

3 na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya,

na asiyemsingizia mwenzake,

4 ambaye humdharau mtu mbaya,

lakini huwaheshimu wale wamwogopao Bwana,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-