Publicidade

Salmos 28

Kuomba Msaada
Zaburi ya Daudi.

1 Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu;

usiwe kwangu kama kiziwi.

Kwa sababu ukinyamaza

nitafanana na walioshuka shimoni.

2 Sikia kilio changu unihurumie

ninapokuita kwa ajili ya msaada,

niinuapo mikono yangu kuelekea

Patakatifu pa Patakatifu pako.

3 Usiniburute pamoja na waovu,

pamoja na hao watendao mabaya,

ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,

lakini mioyoni mwao wameficha chuki.

4 Walipe sawasawa na matendo yao,

sawasawa na matendo yao maovu;

walipe sawasawa na kazi za mikono yao,

uwalipe wanavyostahili.

5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana,

na yale ambayo mikono yake imetenda,

atawabomoa na kamwe

hatawajenga tena.

6 Bwana asifiwe,

kwa maana amesikia kilio changu

nikimwomba anihurumie.

7 Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,

moyo wangu umemtumaini yeye,

nami nimesaidiwa.

Moyo wangu unarukaruka kwa furaha

nami nitamshukuru kwa wimbo.

8 Bwana ni nguvu ya watu wake,

ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.

9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;

uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-