Publicidade

Salmos 113

Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake

1 Msifuni Bwana.

Enyi watumishi wa Bwana msifuni,

lisifuni jina la Bwana.

2 Jina la Bwana na lisifiwe,

sasa na hata milele.

3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,

jina la Bwana linapaswa kusifiwa.

4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote,

utukufu wake juu ya mbingu.

5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu,

Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,

6 ambaye huinama atazame chini

aone mbingu na nchi?

7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,

na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,

8 huwaketisha pamoja na wakuu,

pamoja na wakuu wa watu wake.

9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,

akiwa mama watoto mwenye furaha.

Msifuni Bwana.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-