Publicidade

Salmos 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu
Wimbo wa kwenda juu.

1 Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili wenye haki wasije wakatumia

mikono yao kutenda ubaya.

4 Ee Bwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-