Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 123

Kuomba Rehema

Wimbo wa kwenda juu.

1 Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.

2 Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mtumishi wa kike

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyo Bwana Mungu wetu,

mpaka atakapotuhurumia.

3 Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4 Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também