Publicidade

Salmos 129

Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli
Wimbo wa kwenda juu.

1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2 wamenionea mno tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3 Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4 Lakini Bwana ni mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5 Wale wote waichukiao Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6 Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8 Wale wapitao karibu na wasiseme,

"Baraka ya Bwana iwe juu yako;

tunakubariki katika jina la Bwana."

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-