Utangulizi: Kusudi Na Kiini
1 Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2 Kwa kupata hekima na nidhamu;
kwa kufahamu maneno ya busara;
3 kwa kujipatia nidhamu na busara,
kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
4 huwapa busara wajinga,
maarifa na akili kwa vijana;