7Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
18uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwa nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
27Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini."
4Kisha watamlilia Mwenyezi Mungu,lakini hatawajibu.Wakati huo atawaficha uso wakekwa sababu ya uovu waliotenda.
5Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu:"Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu,mtu akiwalisha,wanatangaza ‘amani’;kama hakufanya hivyo,wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
11Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa,na makuhani wake wanafundisha kwa malipo,nao manabii wake wanatabiri kwa fedha.Hata hivyo wanamwegemea Mwenyezi Mungu na kusema,"Je, Mwenyezi Mungu si yumo miongoni mwetu?Hakuna maafa yatakayotupata."
1"Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja," asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
7Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi," asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni."Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
10Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili," asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, "nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi hata mkose nafasi ya kutosha.
10Mimi na ndugu zangu na watu wangu tunawakopesha watu fedha na nafaka. Lakini jambo hili la kutoza riba likome!
15Lakini watawala wa mwanzoni, wale walionitangulia, waliwalemea watu na kuchukua kutoka kwao shekeli arobaini za fedha5:15 Shekeli 40 za fedha ni sawa na gramu 456., pamoja na chakula na mvinyo. Wasaidizi wao pia walijifanya wakuu juu ya watu. Lakini kwa kumheshimu Mungu sikufanya hivyo.
19Unikumbuke kwa fadhili, Ee Mungu wangu, kwa yote niliyofanya kwa ajili ya watu hawa.
4Bwana Mungu Mwenyezi amenipa ulimi uliofundishwa,ili kujua neno limtegemezalo aliyechoka.Huniamsha asubuhi kwa asubuhi,huamsha sikio langu lisikie kama mtu afundishwaye.
9Ni Bwana Mungu Mwenyezi anisaidiaye mimi.Ni nani huyo atakayenihukumu?Wote watachakaa kama vazi,nondo watawala wawamalize.
10Ni nani miongoni mwenu amchaye Mwenyezi Mungu,na kulitii neno la mtumishi wake?Yeye atembeaye gizani,yeye asiye na nuru,na alitumainie jina la Mwenyezi Mungu,na amtegemee Mungu wake.
11Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Mwenyezi Mungu, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
16Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi aliweka kumbukumbu;
1Al-Yasa akasema, "Sikiliza neno la Mwenyezi Mungu. Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja7:1 Kipimo kimoja cha unga ni sawa na kilo 3. cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha7:1 Shekeli moja ni sawa na gramu 11., na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria."
4Tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kambi ya Waaramu, tujisalimishe. Wakituacha hai, tutaishi; wakituua, basi na tufe."
16Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Mwenyezi Mungu alivyokuwa amesema.
4Unapomwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza. Yeye hafurahii wapumbavu; timiza nadhiri yako.
6Usiruhusu kinywa chako kukuingiza dhambini. Tena usijitetee mbele ya huyo mjumbe wa hekaluni, ukisema, "Niliweka nadhiri kwa makosa." Kwa nini Mungu akasirike kwa ajili ya yale unayosema na kuiharibu kazi ya mikono yako?
7Kuota ndoto kwingi na maneno mengi ni ubatili. Kwa hiyo mche Mungu.
8Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Mwenyezi Mungu yeye aliwatia mkononi mwako.
9Kwa kuwa macho ya Mwenyezi Mungu yanazunguka dunia yote ili kuwatia nguvu wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu, na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita."
5wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu kama hao.
8Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo watu hawa hupingana na kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
17ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
8Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wanaosimama mbele yako daima na kusikia hekima yako!
9Ahimidiwe Mwenyezi Mungu, Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka kwenye kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Mwenyezi Mungu wa milele kwa Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu."
23Mfalme Sulemani alikuwa na utajiri mkubwa na mwenye hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
2Mwenyezi Mungu asema,"Nitafagia kila kitukutoka uso wa dunia.
7Nyamazeni mbele za Bwana Mungu Mwenyezi,kwa maana siku ya Mwenyezi Mungu iko karibu.Mwenyezi Mungu ameandaa dhabihu,amewaweka wakfu wale aliowaalika.
17Nitawaletea watu dhiki,nao watatembea kama vipofu,kwa sababu wametenda dhambidhidi ya Mwenyezi Mungu.Damu yao itamwagwa kama vumbina matumbo yao kama kinyesi.
5mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Haruni.
28ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Mwenyezi Mungu, Mungu wangu, ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.