8 Kulikuwa na mtu aliye peke yake,
hakuwa na mwana wala ndugu.
Hapakuwa na mwisho wa kazi yake;
hata hivyo macho yake
hayakutosheka na utajiri wake.
Aliuliza, "Ninajitaabisha hivi kwa ajili ya nani,
nami kwa nini ninajinyima kufurahia?"
Hili pia ni ubatili,
ni shughuli yenye taabu!