5 Nanyi mmesahau yale maneno ya kuwaonya yanayowataja ninyi kuwa wana, yakisema:
"Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi Mungu,
wala usikate tamaa akikukemea,
6 kwa sababu Mwenyezi Mungu huwaadibisha wale anaowapenda,
na humwadhibu kila mmoja
anayemkubali kuwa mwana."