Publicidade

Joel 1

1 Neno la Mwenyezi Mungu ambalo lilimjia Yoeli mwana wa Pethueli.

Kuvamiwa wa nzige

2 Sikilizeni hili, enyi wazee;

sikilizeni, ninyi nyote mnaoishi katika nchi.

Je, jambo kama hili lilishawahi kutokea

katika siku zenu au katika siku za babu zenu?

3 Waelezeni watoto wenu,

na watoto wenu wawaambie watoto wao,

na watoto wao kwa kizazi kitakachofuata.

4 Kilichosazwa na kundi la tunutu

nzige wakubwa wamekula,

kilichosazwa na nzige wakubwa

parare wamekula,

kilichosazwa na parare

madumadu wamekula.

5 Amkeni, enyi walevi, mlie!

Pigeni yowe enyi wanywaji wote wa mvinyo,

pigeni yowe kwa sababu ya mvinyo mpya,

kwa kuwa mmenyang’anywa

kutoka midomoni mwenu.

6 Taifa limevamia nchi yangu,

lenye nguvu tena lisilo na idadi;

lina meno ya simba,

magego ya simba jike.

7 Limeharibu mizabibu yangu

na kuangamiza mitini yangu.

Limebambua magome yake

na kuyatupilia mbali,

likayaacha matawi yake yakiwa meupe.

8 Omboleza kama bikira aliyevaa gunia

akimwomboleza mume wa ujana wake.

9 Sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimekatiliwa mbali kutoka nyumba ya Mwenyezi Mungu.

Makuhani wanaomboleza,

wale wanaohudumu mbele za Mwenyezi Mungu.

10 Mashamba yameharibiwa,

ardhi imekauka;

nafaka imeharibiwa,

mvinyo mpya umekauka,

mafuta yamekoma.

11 Kateni tamaa, enyi wakulima,

lieni, enyi mlimao mizabibu;

huzunikeni kwa ajili ya ngano na shayiri,

kwa sababu mavuno ya shambani yameharibiwa.

12 Mzabibu umekauka

na mtini umenyauka;

mkomamanga, mtende na mtofaa,

miti yote shambani, imekauka.

Hakika furaha yote ya mwanadamu

imeondoka.

Wito wa kuomboleza

13 Vaeni gunia, enyi makuhani, mwomboleze;

pigeni yowe, enyi mnaohudumu madhabahuni.

Njooni, vaeni gunia usiku kucha,

enyi mnaohudumu mbele za Mungu wangu;

kwa kuwa sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji

zimezuiliwa kufika katika nyumba ya Mungu wenu.

14 Tangazeni saumu takatifu;

liiteni kusanyiko takatifu.

Waiteni wazee

na wote wanaoishi katika nchi

waende katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu,

wakamlilie Mwenyezi Mungu.

15 Ole kwa siku hiyo!

Kwa kuwa siku ya Mwenyezi Mungu iko karibu;

itakuja kama uharibifu

kutoka kwa Mwenyezi.

16 Je, chakula hakikukatiliwa mbali

mbele ya macho yetu:

furaha na shangwe

kutoka nyumba ya Mungu wetu?

17 Mbegu zinakauka

chini ya mabonge ya udongo.

Maghala yameachwa katika uharibifu,

maghala ya nafaka yamebomolewa,

kwa maana hakuna nafaka.

18 Jinsi gani ng’ombe wanavyolia!

Makundi ya mifugo yanahangaika

kwa sababu hawana malisho;

hata makundi ya kondoo yanateseka.

19 Kwako, Ee Mwenyezi Mungu, naita,

kwa kuwa moto umeteketeza

malisho ya mbugani

na miali ya moto imeunguza

miti yote shambani.

20 Hata wanyama pori wanakuonea shauku;

vijito vya maji vimekauka,

na moto umeteketeza

malisho yote ya mbugani.

Veja também

Publicidade
Joel
Ver todos os capítulos de Joel
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_14-04-22-