7 "Lakini amebarikiwa mtu anayemtumaini Mwenyezi Mungu,
ambaye matumaini yake ni katika Mwenyezi Mungu.
8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji
uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.
Hauogopi wakati wa joto ujapo;
majani yake ni mabichi daima.
Hauna hofu katika mwaka wa ukame
na hautaacha kuzaa matunda."