Publicidade

Jeremias 18

Katika nyumba ya mfinyanzi

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Mwenyezi Mungu: 2 "Shuka uende hadi nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu." 3 Kwa hiyo nikashuka hadi nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake. 4 Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake; hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kwa namna alivyoona ni vyema machoni pake.

5 Kisha neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema: 6 "Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?" asema Mwenyezi Mungu. "Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-