4 "Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?
Niambie, kama unafahamu.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?
Hakika wewe unajua!
Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,
au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,
na malaika wote walipokuwa wakishangilia kwa furaha?
8 "Ni nani aliyeifungia bahari milango
ilipopasuka kutoka tumbo,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,
na kuyafungia katika giza nene,
10 nilipoamuru mipaka yake,
na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika hapa, wala si zaidi;
hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?