Wanafunzi wa kwanza wa Isa
16 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa walikuwa wavuvi. 17 Isa akawaambia, "Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu." 18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.