Pular para o conteúdo
Publicidade

Marcos 5

Isa amponya mtu mwenye pepo mchafu

1 Isa na wanafunzi wake wakafika upande wa pili wa ziwa, wakaingia katika nchi ya Wagerasi. 2 Isa alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini, akakutana naye. 3 Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo. 4 Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia. 5 Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.

6 Alipomwona Isa kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake. 7 Akapaza sauti kwa nguvu akisema, "Una nini nami, Isa, Mwana wa Mungu5:7 Yaani Mwana wa asili moja na Mwenyezi Mungu (Yohana 1:1-2), wa kiroho, bali si wa kimwili. Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!" 8 Kwa kuwa Isa alikuwa amemwambia, "Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!"

9 Isa akamuuliza, "Jina lako ni nani?"

Akamjibu, "Jina langu ni Legioni5:9 maana yake Jeshi, kwa kuwa tuko wengi." 10 Akamsihi Isa sana asiwapeleke nje ya nchi ile.

11 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima. 12 Wale pepo wachafu wakamsihi Isa wakisema, "Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie." 13 Basi Isa akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao elfu mbili, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.

14 Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakaenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia.

Veja também