35 Mchana ulipokuwa umeendelea sana, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, nazo saa zimeenda sana. 36 Waage watu ili waende mashambani na vijijini jirani, wakajinunulie chakula."
37 Lakini Isa akawajibu, "Ninyi wapeni chakula."
Wakamwambia, "Je, twende tukanunue mikate ya dinari mia mbili6:37 Dinari moja ilikuwa kama mshahara wa kibarua wa siku moja. ili tuwape watu hawa wale?"
38 Akawauliza, "Kuna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie."
Walipokwisha kujua, wakarudi, wakamwambia, "Kuna mikate mitano na samaki wawili."
39 Kisha Isa akawaamuru wawaketishe watu makundi makundi kwenye majani, 40 nao wakaketi kwenye vikundi vya watu mia mia, na wengine hamsini hamsini. 41 Isa akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi wake ili wawagawie wale watu wote. Pia akawagawia wote wale samaki wawili. 42 Watu wote wakala, wakashiba. 43 Nao wanafunzi wake wakakusanya vipande vilivyosalia vya mikate na samaki, wakajaza vikapu kumi na viwili. 44 Idadi ya wanaume waliokula walikuwa elfu tano.