Publicidade

Miquéias 5

Mtawala aliyeahidiwa kutoka Bethlehemu

1 Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi,

kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.

Watampiga mtawala wa Israeli

shavuni kwa fimbo.

2 "Lakini wewe, Bethlehemu Efrata,

ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,

kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu

yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,

ambaye asili yake ni kutoka zamani,

kutoka milele."

3 Kwa hiyo Israeli utaachwa

hadi mwanamke aliye na uchungu atakapozaa mwana,

na ndugu zake wengine warudi

kujiunga na Waisraeli.

4 Atasimama na kulichunga kundi lake

katika nguvu ya Mwenyezi Mungu,

katika utukufu wa jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wake.

Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo

ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.

5 Naye atakuwa amani yao.

Ukombozi na uharibifu

Mwashuru atakapovamia nchi yetu

na kupita katika ngome zetu,

tutawainua wachungaji saba dhidi yake,

hata viongozi wanane wa watu.

6 Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,

nchi ya Nimrodi kwa upanga.

Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru

atakapoivamia nchi yetu

na kuingia katika mipaka yetu.

7 Mabaki ya Yakobo yatakuwa

katikati ya mataifa mengi

kama umande kutoka kwa Mwenyezi Mungu,

kama manyunyu juu ya majani,

ambayo hayamngoji mtu

wala kukawia kwa mwanadamu.

8 Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,

katikati ya mataifa mengi,

kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,

kama mwana simba miongoni

mwa makundi ya kondoo,

ambaye anaumiza vibaya na kuwararua

kila anapopita katikati yao,

wala hakuna awezaye kuokoa.

9 Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,

nao adui zako wote wataangamizwa.

10 "Katika siku ile," asema Mwenyezi Mungu,

"nitaangamiza farasi wenu kati yenu,

na kubomoa magari yenu ya vita.

11 Nitaiangamiza miji ya nchi yenu,

na kuziangusha chini ngome zenu zote.

12 Nitaangamiza uchawi wenu,

na hamtapiga tena ramli.

13 Nitaangamiza sanamu zenu,

na mawe yenu ya ibada yatoke kati yenu;

hamtasujudia tena

kazi ya mikono yenu.

14 Nitang’oa nguzo za Ashera kati yenu,

na kubomoa miji yenu.

15 Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu,

kwa mataifa ambayo hayajanitii."

Veja também

Publicidade
Miquéias
Ver todos os capítulos de Miquéias
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_10-32-54-