Pular para o conteúdo
Publicidade

Cânticos 7

Maelezo ya wasifu

1 Zab 45:13 Binti wa kimalkia, jinsi ulivyo mzuri

Hatua zako katika mitarawanda.

Mapaja yako ya mviringo ni kama johari,

Kazi ya mikono ya fundi stadi;

2 Kitovu chako ni kama bakuli la mviringo,

Na isikose divai iliyochanganyika;

Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano,

Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;

3 Wim 4:5 Matiti yako mawili ni kama wanapaa wawili,

Ambao ni mapacha ya paa;

4 Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe;

Macho yako kama viziwa vya Heshboni,

Karibu na mlango wa Beth-rabi;

Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,

Unaoelekea Dameski;

5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli,

Na nywele za kichwa chako kama urujuani,

Mfalme amenaswa na mashungi yake.

6 Jinsi yalivyo mazuri, yalivyo matamu,

Mapenzi katikati ya anasa!

7 Kimo chako kimefanana na mtende,

Na matiti yako na vichala.

8 Nilisema, Nitapanda huo mtende,

Na kuyashika makuti yake.

Matiti yako na yawe kama vichala vya mzabibu,

Na harufu ya pumzi yako kama mapera;

9 Na kinywa chako kama divai iliyo bora,

Kwa mpendwa wangu inashuka taratibu,

Ikitiririka midomoni mwao walalao.

10 Wim 2:16;Gal 2:20;Zab 45:11 Mimi ni wake mpendwa wangu,

Na shauku yake ni juu yangu.

11 Njoo, mpendwa wangu, twende mashambani,

Tufanye maskani katika vijiji.7:11 Au, penye maua ya mhina.

12 Wim 6:11;4:16;Zab 63:3-8;73:25 Twende mapema hadi mashamba ya mizabibu,

Tuone kama mzabibu umechanua,

Na maua yake yamefunuka;

Kama mikomamanga imetoa maua;

Huko nitakupa upendo wangu.

13 Mwa 30:14;Wim 5:1;Mt 13:52;Yn 15:8 Mitunguja hutoa harufu yake;

Juu ya milango yetu yako matunda mazuri,

Mapya na ya kale, ya kila namna,

Niliyokuwekea, mpendwa wangu.

Veja também