16 Wakamtia wivu kwa miungu migeni,
Wakamkasirisha kwa machukizo.
17 1 Kor 10:20Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu,
Kwa miungu wasiyoijua,
Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu,
Ambayo baba zenu hawakuiogopa.
18 Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa,
Mungu aliyekuzaa umemsahau.