Pular para o conteúdo
Publicidade

Waefeso 1

Sala ya Paulo

15 Kol 1:4,9Kwa sababu hiyo mimi nami, tangu nilipopata habari za imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa watakatifu wote, 16 Kol 1:3siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, 17 Kol 1:10Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; 18 Kum 33:3,4;Efe 4:4;Kol 1:5,11macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; 19 2 Kor 13:4;Kol 1:11;2:12na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; 20 Zab 110:1aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka katika mkono wake wa kulia katika ulimwengu wa roho; 21 Kol 1:16;2:10juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na utawala, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22 Zab 8:6;Mt 28:18;Efe 4:15;Kol 1:18akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23 Rum 12:5;Kol 1:19;1 Kor 12:27;Efe 4:10ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também