8 Mungu akamwambia Nuhu, na wanawe pamoja naye, akisema, 9 Tazama, nilithibitisha agano langu nanyi; tena na uzao wenu baada yenu; 10 Mwa 8:1tena na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, ndege, na mnyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu katika nchi pamoja nanyi; wote wanaotoka katika safina, hata kila kilicho hai katika nchi. 11 2 Pet 3:5Na agano langu nitalithibitisha nanyi; wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika, baada ya hayo, kuiharibu nchi.
Publicidade