7 Zab 2:12;Mit 16:20Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA,
Ambaye BWANA ni tumaini lake.
8 Zab 1:3Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji,
Uenezao mizizi yake karibu na mto;
Hautaona hofu wakati wa joto ujapo,
Bali jani lake litakuwa bichi;
Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua,
Wala hautaacha kuzaa matunda.