1 Neno la BWANA lililomjia Yeremia, nabii, kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajashambulia Gaza.
2 BWANA asema hivi, Tazama, maji yanatokea katika pande za kaskazini, nayo yatakuwa mto ufurikao, nayo yataifunika nchi, na kila kitu kilichomo, huo mji na wote wakaao ndani yake; nao watu watalia na watu wote wakaao katika nchi wataomboleza. 3 Kwa sababu ya kishindo cha kukanyaga kwa kwato za farasi wake walio hodari, kwa sababu ya mwendo wa mbio mbio wa magari yake ya vita; kwa sababu ya mngurumo wa magurudumu yake, hao akina baba hawatazami nyuma ili kuwaangalia watoto wao, kwa kuwa mikono yao ni dhaifu; 4 kwa sababu ya siku ijayo kuwaangamiza Wafilisti wote, kukatilia mbali kila msaidizi wa Tiro na Sidoni asaliaye; maana BWANA atawaharibu Wafilisti, mabaki ya kisiwa cha Kaftori.
5 Upaa umeupata Gaza;
Ashkeloni umenyamazishwa
Mabaki ya bonde lao;
Hata lini utajikatakata?
6 Ee upanga wa BWANA,
Siku ngapi zitapita kabla hujatulia?
Ujitie katika ala yako;
Pumzika, utulie.
7 Utawezaje kutulia,
Ikiwa BWANA amekupa agizo?
Juu ya Ashkeloni na juu ya pwani,
Ndipo alipoyaamuru hayo.