Publicidade

Jeremias 47

Hukumu juu ya Wafilisti

1 Neno la BWANA lililomjia Yeremia, nabii, kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajashambulia Gaza.

2 BWANA asema hivi, Tazama, maji yanatokea katika pande za kaskazini, nayo yatakuwa mto ufurikao, nayo yataifunika nchi, na kila kitu kilichomo, huo mji na wote wakaao ndani yake; nao watu watalia na watu wote wakaao katika nchi wataomboleza. 3 Kwa sababu ya kishindo cha kukanyaga kwa kwato za farasi wake walio hodari, kwa sababu ya mwendo wa mbio mbio wa magari yake ya vita; kwa sababu ya mngurumo wa magurudumu yake, hao akina baba hawatazami nyuma ili kuwaangalia watoto wao, kwa kuwa mikono yao ni dhaifu; 4 kwa sababu ya siku ijayo kuwaangamiza Wafilisti wote, kukatilia mbali kila msaidizi wa Tiro na Sidoni asaliaye; maana BWANA atawaharibu Wafilisti, mabaki ya kisiwa cha Kaftori.

5 Upaa umeupata Gaza;

Ashkeloni umenyamazishwa

Mabaki ya bonde lao;

Hata lini utajikatakata?

6 Ee upanga wa BWANA,

Siku ngapi zitapita kabla hujatulia?

Ujitie katika ala yako;

Pumzika, utulie.

7 Utawezaje kutulia,

Ikiwa BWANA amekupa agizo?

Juu ya Ashkeloni na juu ya pwani,

Ndipo alipoyaamuru hayo.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-22_10-02-25-