Publicidade

Confiabilidade

Por Bíblia Online

A confiabilidade de Deus é absoluta. Ele é fiel em todas as suas promessas, constante em seu amor e seguro em seu caráter. Podemos confiar nele completamente.

Deus é fiel

O Senhor é fiel em todas as suas palavras e bondoso em todos os seus atos. Grande é a sua fidelidade!

Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii,

Kwa kuwa rehema zake hazikomi.

Ni mpya kila siku asubuhi;

Uaminifu wako ni mkuu.

BWANA yuko karibu na wote wamwitao,

Wote wamwitao kwa uaminifu.

BWANA atanitimizia malengo yake kwangu;

Ee BWANA, fadhili zako ni za milele;

Usiiache kazi ya mikono yako.

Bali fadhili za BWANA ni kwa wamchao

Tangu milele hata milele,

Na haki yake ni kwa vizazi vyote;

Kwa wale walishikao agano lake,

Na kuyakumbuka maagizo yake ili wayafanye.

Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao,

Wazingojeao fadhili zake.

Kwa kuwa BWANA hupenda haki,

Wala hawaachi watauwa wake.

Wao hulindwa milele,

Bali mzawa wa wasio haki ataharibiwa.

Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda kutoka kwa yule mwovu.

Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili muweze kustahimili.

Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hadi vizazi elfu;

Naye BWANA, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.

Caráter de Deus

Toda boa dádiva vem do alto. O Senhor é bom e sua misericórdia dura para sempre. Nele podemos descansar.

Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.

Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema,

Umekuwa tayari kusamehe,

Na mwingi wa fadhili,

Kwa watu wote wakuitao.

Maana hushibisha nafsi yenye shauku,

Na nafsi yenye njaa huijaza mema.

Nami nitaimba juu ya nguvu zako,

Nitaimba kwa furaha juu ya fadhili zako asubuhi.

Maana umekuwa ngome yangu,

na kimbilio wakati wa mateso yangu.

Umtwike BWANA mzigo wako naye atakutegemeza,

Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.

Hatauacha mguu wako usogezwe;

Akulindaye hatasinzia;

Integridade e confiança

Eu sou o Alfa e o Ômega — Deus é o mesmo ontem, hoje e sempre. Fiel em o que realizou e realizará por cada filho.

Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.

Wewe, BWANA, unadumu milele;

Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.

Sifa kwa kukombolewa katika udhalimu

Ee BWANA, wewe u Mungu wangu;

Nitakutukuza na kulihimidi jina lako;

Kwa kuwa umetenda mambo ya ajabu,

Mashauri ya kale, kwa uaminifu na kweli.

Haja ya mwanadamu ni hisani yake;

Ni afadhali maskini kuliko mwongo.

Mwenye udaku hupitapita akifunua siri;

Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza

Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.

Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.

Hata sasa hamjaomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_12-11-46-