1 Zab 119:46 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,
Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
2 1 Fal 8:29;Zab 5:7;Dan 6:10;Yon 2:7;Isa 42:21 Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu,
Nitalishukuru jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
na jina lako juu ya vyote.
3 2 Kor 12:9;Zek 10:12 Siku ile niliyokuita uliniitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.
4 Ee BWANA, wafalme wote wa dunia watakushukuru,
Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.
5 Naam, wataziimba njia za BWANA,
Kwa maana utukufu wa BWANA ni mkuu.
6 Mit 3:34;Yak 4:6 Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu,
Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
7 Zab 23:3 Nijapopitia katika shida,
Unanilinda juu ya hasira ya adui zangu,
Unaunyosha mkono wako,
Na mkono wako wa kulia unaniokoa.
8 Zab 57:2;Flp 1:6 BWANA atanitimizia malengo yake kwangu;
Ee BWANA, fadhili zako ni za milele;
Usiiache kazi ya mikono yako.