Dificuldades
As dificuldades são parte da vida, mas Deus é refúgio certo em todo tempo de angústia. A Bíblia promete que nenhuma adversidade pode separar os filhos de Deus do seu amor.
Deus é refúgio
Deus é nosso refúgio e fortaleza, socorro bem presente nas angústias. Nada poderá nos separar do amor de Cristo.
Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi,
Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
Maji yake yajapovuma na kuumuka,
Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.
Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu nitakayemtumaini.
Enyi watu, mtumainini sikuzote,
Ifunueni mioyo yenu mbele zake;
Mungu ndiye kimbilio letu.
BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa,
Naam, ngome kwa nyakati za shida.
Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe,
Maana Wewe, BWANA hukuwaacha wakutafutao.
Wewe ndiwe ukitawalaye kiburi cha bahari.
Mawimbi yake yainukapo, wewe unayatuliza.
Kupita sauti ya maji mengi, maji makuu,
Kupita mawimbi ya bahari yaumkayo,
BWANA Aliye Juu ndiye mwenye ukuu.
Huituliza dhoruba, ikawa shwari,
Mawimbi yake yakanyamaza.
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba,
Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa,
Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa.
Lakini katika mambo hayo yote sisi ni zaidi ya washindi, kupitia kwake yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Provisão nas dificuldades
O Senhor provê mesmo nos tempos mais difíceis. Ele sustentou Elias, protegeu Israel e cuida dos seus com fidelidade eterna.
Lile pipa la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa kinywa cha Eliya.
Alitandaza wingu liwe kifuniko,
Na moto ili uwaangazie usiku.
Walimwomba naye akaleta kware,
Na kuwashibisha chakula cha mbinguni.
Akaufunua mwamba, kukabubujika maji,
Yakapita jangwani kama mto.
Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,
Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa
Wala mzawa wake akiomba chakula.
BWANA huwatunza waaminifu,
Na urithi wao utakuwa wa milele.
Hawataaibika wakati wa ubaya,
Na siku za njaa watashiba.
Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;
Maana umekuwa ngome ya maskini,
Ngome ya mhitaji katika dhiki yake,
Mahali pa kukimbilia wakati wa tufani,
Na kivuli wakati wa joto;
Wakati kishindo cha watu wakatili kilipokuwa,
Kama dhoruba ipigayo ukuta.
Kisha kutakuwa na hema kuwa uvuli wakati wa mchana kwa sababu ya joto, na kuwa mahali pa kukimbilia na kujificha wakati wa tufani na mvua.
Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.
Força nas provas
Em tudo somos atribulados, mas não esmagados. O Senhor é bom e é fortaleza no dia da angústia — Ele conhce os seus.
Pande zote twateseka, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi;
BWANA ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.
Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito;
Na hilo wingu halipasuki chini yake.
Husitiri uso wa kiti chake cha enzi,
Na kulitandaza wingu lake juu yake.
Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji,
Hata hapo mwanga na giza vinapopakana.
Utafichwa na mapigo ya ulimi;
Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.
Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu. Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?
Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa katika tanuri, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba? Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini.
Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.