1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Mit 25:11 Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo!
Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu!
3 1 Kor 2:4 Jinsi ulivyomshauri huyo asiye na hekima!
Na kutangaza ujuzi wa kweli kwa wingi!
4 Je! Umetamka maneno kwa nani?
Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?
5 Hao waliokufa watetemesha
Chini ya maji na hao wakaamo humo.
6 Zab 139:8;Mit 15:11;Isa 14:9;Amo 9:2;Ebr 4:13 Kaburi li wazi mbele yake,
Uharibifu nao hauna kifuniko.
7 Zab 24:1,2 Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu,
Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.
8 Mit 30:4 Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito;
Na hilo wingu halipasuki chini yake.
9 Husitiri uso wa kiti chake cha enzi,
Na kulitandaza wingu lake juu yake.
10 Yer 5:22 Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji,
Hata hapo mwanga na giza vinapopakana.
11 Nguzo za mbingu zatetemeka,
Na kustaajabu kwa kukemea kwake.
12 Kut 14:21;Isa 51:15;Zab 29:10;74:13 Huichafua bahari kwa uwezo wake,
Na kumtema Rahabu kwa akili zake.
13 Zab 33:6 Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake;
Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.
14 Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake;
Na jinsi yalivyo madogo manong’ono tusikiayo katika habari zake!
Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuzielewa?