Pular para o conteúdo
Publicidade

Ayubu 27

Ayubu ashikilia uelekevu wake

1 Kisha Ayubu akaendelea na hoja yake, na kusema,

2 Ayu 34:5 Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu;

Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;

3 (Kwa kuwa uhai wangu ungali mzima ndani yangu,

Na Roho ya Mungu iko katika pua yangu;)

4 Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki,

Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.

5 Ayu 13:15 Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki;

Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.

6 Ayu 2:3;Mdo 24:16 Haki yangu naishika sana, wala sitaiacha;

Moyo wangu hautanisuta wakati nikiwapo hai.

7 Adui yangu na awe kama huyo mwovu,

Na mpinzani wangu awe kama asiye haki.

8 Mt 16:26 Maana tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida,

Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?

9 Mit 1:28;Isa 1:15;Mik 3:4;Zek 7:13;Yak 4:3 Je! Mungu atakisikia kilio chake,

Taabu zitakapomfikia?

10 Ayu 22:26 Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi,

Na kumlingana Mungu nyakati zote?

11 Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu;

Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.

12 Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe;

Mbona basi mmebatilika kabisa?

13 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu,

Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.

14 Kum 28:32,41;Est 9:10;2 Fal 10:6-10 Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga;

Na wazao wake hawatashiba chakula.

15 Zab 78:64 Hao watakaosalia kwake watakufa kwa maradhi mabaya,

Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.

16 Ajapokusanya fedha kama mavumbi,

Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;

17 Mit 28:8;Mhu 2:26 Yumkini kuyatengeza, lakini wenye haki watayavaa,

Nao wasio na hatia watazigawanya hizo fedha.

18 Omb 2:6 Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu,

Na kama kibanda afanyacho mlinzi.

19 Hes 20:26 Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho;

Hufunua macho yake, naye hayuko.

20 Vitisho vyampata kama maji mengi;

Dhoruba humwiba usiku.

21 Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka;

Na kumkumba atoke mahali pake.

22 Kwani Mungu atamtupia asimhurumie;

Angependa kuukimbia mkono wake.

23 Watu watampigia makofi,

Na kumzomea atoke mahali pake.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também