Bildadi anena: Mtu awezaje kuwa mwenye haki mbele za Mungu
1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,
2 Enzi na hofu zi pamoja na Mungu;
Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.
3 Je! Majeshi yake yahesabika?
Ni nani asiyetokewa na mwanga wake?
4 Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu?
Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?
5 Tazama, hata mwezi hauangazi,
Wala nyota si safi machoni pake;
6 Seuze mtu, aliye mdudu!
Na mwanadamu, ambaye ni buu!