Elihu alaani haki ya ubinafsi
1 Tena Elihu akajibu na kusema,
2 Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako,
Au je! Wasema, Ni haki yangu mbele za Mungu,
3 Maana wasema, Kutakuwa na faida gani kwako wewe?
Tena, Nitapata faida gani, kuliko nikifanya dhambi?
4 Mimi nitakujibu,
Na hawa wenzio pamoja nawe.
5 Ziangalie mbingu ukaone;
Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.
6 Ayu 22:2-3 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake?
Ikiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7 Mit 9:12;Rum 11:35 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani?
Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe;
Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
9 Kut 2:23;Neh 5:5;Ayu 24:12;Zab 12:5;Lk 18:3-7 Kwa sababu ya wingi wa dhuluma wao hulia;
Walilia msaada kwa sababu ya mkono wa wakuu.
10 Mhu 12:1;Isa 51:13;1 Pet 4:19;Zab 42:8;Mdo 16:25 Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu,
Awapaye nyimbo wakati wa usiku;
11 Ayu 32:8;Zab 8:6;1 Yoh 5:20 Atufundishaye zaidi ya wanyama wa nchi,
Na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?
12 Mit 1:28 Hulia huko, lakini hapana ajibuye,
Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
13 Hakika Mungu hatasikia ubatili,
Wala Mwenyezi hatauangalia.
14 Sembuse usemapo wewe ya kuwa humwangalii,
Hiyo kesi i mbele yake, nawe wamngojea!
15 Lakini sasa, kwa sababu yeye hakukujia katika hasira zake,
Wala hauzingatii sana makosa;
16 Ayu 34:35,37 Ndiposa Ayubu hufunua kinywa chake kwa ubatili;
Huongeza maneno pasipo maarifa.