Ayubu asisitiza kuwa hana hatia
1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Nimesikia maneno mengi mfano wa hayo;
Ninyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha.
3 Je! Maneno yasiyo faida yatakuwa na mwisho?
Au, kuna nini kinachokukasirisha, hata ukajibu?
4 2 Fal 19:21;Zab 22:7;Yer 18:16;Omb 2:15 Mimi nami ningeweza kunena kama ninyi;
Kama roho zenu zingekuwa mahali pa roho yangu,
Ningeweza kutunga maneno juu yenu,
Na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu,
Na maliwazo ya midomo yangu yangewatuliza.
6 Nijapokuwa nanena, huzuni yangu haitulizwi;
Nijapokuwa najizuia, nimepunguziwa kitu gani?
7 Lakini sasa amenichokesha;
Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.
8 Umenishika sana, na kuwa ushahidi juu yangu;
Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.
9 Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea;
Amesagasaga meno juu yangu;
Mtesi wangu hunikazia macho makali.
10 Zab 22:13;1 Fal 22:24;Omb 3:30;Mik 5:1;Mt 26:67;Yn 18:22;Mdo 23:2;Zab 35:15 Wamenifumbulia vinywa vyao;
Wamenipiga shavuni kwa kunitukana;
Hukutana pamoja juu yangu.
11 Mungu amenitia kwa hao wapotovu,
Na kunitupa mikononi mwao waovu.
12 Nilikuwa katika raha, naye akanivunjavunja;
Naam, amenishika shingo, na kuniponda;
Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.
13 Wapigaji wake wa mishale hunizingira kotekote,
Hunipasua figo zangu, asinihurumie;
Nyonga zangu amezimwaga juu ya nchi.
14 Hunivunja kwa uvunjifu juu ya uvunjifu;
Hunishambulia mfano wa jitu shujaa.
15 Zab 7:5 Nimeshona nguo ya magunia juu ya mwili wangu,
Na nguvu zangu nimezibwaga mavumbini.
16 Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi,
Na giza tupu liko katika kope zangu;
17 Ijapokuwa hakuna udhalimu mikononi mwangu,
Na kuomba kwangu ni safi.
18 Ayu 27:9 Ee nchi, usiifunike damu yangu,
Na kilio changu kisipate mahali pa kupumzika.
19 Ayu 19:25;Rum 1:9 Hata sasa, tazama, shahidi wangu yuko mbinguni.
Na huyo atakayenidhamini yuko juu.
20 Rafiki zangu hunidharau;
Lakini jicho langu humwagia Mungu machozi;
21 Ayu 31:35 Laiti angemtolea mtu hoja mbele ya Mungu,
Amtetee na mwanadamu mbele ya jirani yake.
22 Mhu 12:5 Kwani ikiisha pita miaka michache,
Nitakwenda njia hiyo ambayo sitarudi tena.