Pular para o conteúdo
Publicidade

Ayubu 18

Bildadianena: Mungu huwaadhibu waovu

1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,

2 Je! Hata lini utayawinda maneno kwa mitego?

Fikiri, kisha baadaye tutanena.

3 Ayu 12:7;Zab 73:22 Twahesabiwa kuwa wanyama kwa sababu gani,

Tena kuwa wanajisi machoni pako?

4 Ayu 13:14 Wewe ujiraruaye mwenyewe katika hasira yako,

Je! Dunia itaachwa kwa ajili yako wewe?

Au jabali litaondolewa mahali pake?

5 Ayu 21:17;Mit 13:9 Naam, mwanga wa waovu utazimika,

Wala muali wa moto wake hautang’aa.

6 Mwanga hemani mwake utakuwa giza,

Nayo taa iliyo juu yake itazimwa.

7 Hatua zake za nguvu zitasongwa,

Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.

8 Kwani ametupwa katika wavu na miguu yake mwenyewe,

Naye huenda juu ya matanzi.

9 Tanzi litamshika kisigino chake,

Na mtego utamshika.

10 Amefichiwa tanzi chini,

Na mtego amewekewa njiani.

11 Ayu 6:4;Zab 73:19;Yer 6:25;2 Kor 5:11 Vitisho vitamtia hofu kutoka kila upande,

Na kumfukuza karibu na visigino vyake.

12 Ayu 15:23;1 The 5:3 Nguvu zake zitaliwa na njaa,

Na msiba utakuwa tayari kwa kusita kwake.

13 Utakula via vya mwili wake,

Naam, mzaliwa wa kwanza wa mauti atavila via vyake.

14 Ayu 8:14;Zab 112:10;Mit 10:28;Mt 7:26,27 Atang’olewa katika hema yake aliyokuwa akiitumaini;

Naye atapelekwa kwake mfalme wa vitisho.

15 Mwa 19:24 Katika hema yake hakuna kitakachobaki;

Kiberiti kitamwagwa juu ya makazi yake.

16 Chini, mizizi yake itakaushwa;

Na juu, tawi lake litasinyaa.

17 Zab 34:16;Mit 2:22 Kumbukumbu lake litakoma katika nchi,

Wala hatakuwa na jina mashambani.

18 Atakimbizwa kutoka mwangani hata gizani,

Na kufukuzwa atoke duniani.

19 Isa 14:22;Yer 22:30 Hatakuwa na mwana wala mjukuu kati ya watu wake,

Wala hatasalia mtu hapo alipokaa.

20 Hao wanaokaa magharibi watastaajabia siku yake,

Kama vile wanaokaa mashariki walivyotiwa hofu.

21 Yer 9:3;1 The 4:5;2 The 1:8;Tit 1:16 Hakika ndivyo yalivyo makazi ya wapotovu,

Na hapa ni mahali pake asiyemjua Mungu.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também