Ukuu wa enzi ya Mungu
1 Isa 52:7;Ufu 19:6;Ayu 40:10;Zab 104:1;Isa 59:17 BWANA ametamalaki, amejivika adhama,
BWANA amejivika, ukuu na nguvu, kama mavazi ya kifalme.
Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;
2 Mit 8:22 Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani;
Wewe ndiwe uliye tangu milele.
3 Ee BWANA, mito imepaza,
Mito imepaza sauti zake,
Mito imepaza uvumi wake.
4 Zab 29:10 Kupita sauti ya maji mengi, maji makuu,
Kupita mawimbi ya bahari yaumkayo,
BWANA Aliye Juu ndiye mwenye ukuu.
5 Shuhuda zako ni amini sana;
Utakatifu ndio uifaao nyumba yako,
Ee BWANA, milele na milele.