Publicidade

Meditação

Por Bíblia Online

A meditação na Palavra de Deus é prática espiritual essencial. Diferente da meditação oriental, a meditação bíblica é reflexão profunda sobre as Escrituras — ruminar a Palavra dia e noite.

Meditar na Palavra dia e noite

Bem-aventurado o homem que medita na lei do Senhor de dia e de noite. Ele é como árvore plantada junto a ribeiros de águas.

Njia mbili

Heri mtu yule asiyekwenda

Katika shauri la wasio haki;

Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi;

Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,

Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda kulingana na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

* * *

Sheria yako naipenda mno ajabu,

Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.

Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu,

Kwa maana ninayo sikuzote.

Ninazo akili kuliko waalimu wangu wote,

Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.

Ninao ufahamu kuliko wazee,

Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.

Nitayatafakari maagizo yako,

Na kuziangalia njia zako.

Nitajifurahisha sana kwa amri zako,

Sitalisahau neno lako.

Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako,

Ambayo nimeyapenda.

Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda,

Nami nitazitafakari amri zako.

Naamka kabla ya mapambazuko na kukuomba msaada,

Naweka tumaini langu katika maneno yako.

Nakaa macho usiku kucha,

Ili kuitafakari ahadi yako.

Frutos da meditação

A meditação produz entendimento, alegria e adoração. Quem medita na Palavra encontra direção, paz e renovação espiritual.

Maneno ya kinywa changu,

Na mawazo ya moyo wangu,

Yapate kibali mbele zako, Ee BWANA,

Mwamba wangu, na mwokozi wangu.

Kinywa changu kitanena hekima,

Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara.

Nitayakumbuka matendo ya BWANA;

Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.

Pia nitaitafakari kazi yako yote;

Nitaziwaza habari za matendo yako.

Nimezikumbuka siku za kale,

Nimeyatafakari matendo yako yote,

Naziwaza kazi za mikono yako.

Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu,

Katikati ya hekalu lako.

Nitamwimbia BWANA maadamu ninaishi;

Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;

Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;

Maana furaha yangu hutoka kwa BWANA.

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-