2Kwa nini kutumia fedha kwa kitu ambacho si chakula,na kutaabikia kitu kisichoshibisha?Sikilizeni, nisikilizeni mimi na mle kilicho kizuri,nazo nafsi zenu zitafurahia utajiri wa unono.
6Mtafuteni Bwana maadamu anapatikana;mwiteni maadamu yu karibu.
7Mtu mwovu na aiache njia yake,na mtu mbaya na ayaache mawazo yake.Yeye na amrudie Bwana, naye atamrehemu,arudi kwa Mungu wetu, kwa kuwa atamsamehe bure kabisa.