Rarueni mioyo yenu
12 "Hata sasa," asema Mwenyezi Mungu,
"nirudieni kwa mioyo yenu yote,
kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza."
13 Rarueni mioyo yenu
na siyo mavazi yenu.
Mrudieni Mwenyezi Mungu, Mungu wenu,
kwa maana yeye ndiye mwenye neema
na mwingi wa huruma,
si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo,
huona huruma, hujizuia kuleta maafa.