Faida za hekima
1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 kutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 na kama utaiita busara,
na kuita kwa sauti upate ufahamu,
4 na ukiitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 ndipo utakapoelewa kumcha Mwenyezi Mungu
na kupata maarifa ya Mungu.
6 Kwa maana Mwenyezi Mungu hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.