Pular para o conteúdo
Publicidade

Provérbios 2

Faida za hekima

1 Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

2 kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

3 na kama utaiita busara,

na kuita kwa sauti upate ufahamu,

4 na ukiitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

5 ndipo utakapoelewa kumcha Mwenyezi Mungu

na kupata maarifa ya Mungu.

6 Kwa maana Mwenyezi Mungu hutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

Veja também