Pular para o conteúdo
Publicidade

Provérbios 31

13 Huchagua sufu na kitani,

naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.

14 Yeye ni kama meli za biashara,

akileta chakula chake kutoka mbali.

15 Yeye huamka kukiwa bado giza,

naye huwapa jamaa yake chakula

na wajakazi wake mafungu yao.

16 Huangalia shamba na kulinunua;

kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.

17 Hufanya kazi zake kwa nguvu,

mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.

18 Huona kwamba biashara yake ina faida,

wala taa yake haizimiki usiku.

19 Huweka mikono yake kwenye pia,

navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.

20 Huwanyooshea maskini mikono yake

na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.

Veja também