Onyo dhidi ya uasherati
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako,
wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Yafunge katika moyo wako daima,
yakaze kuizunguka shingo yako.
22 Unapotembea, yatakuongoza;
unapolala, yatakulinda;
unapoamka, yatazungumza nawe.
23 Kwa maana amri hii ni taa,
mafundisho haya ni mwanga,
na maonyo ya nidhamu
ni njia ya uzima,