1Beli anasujudu, Nebo anainama;sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo.Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea,mzigo kwa waliochoka.
4Hata wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye,Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi.Nimewahuluku, nami nitawabeba,nitawahudumia ninyi na kuwaokoa.
11Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye;kutoka nchi ya mbali,mtu atakayetimiza kusudi langu.Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza;lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
3Lakini Wamisri ni wanadamu, wala si Mungu,farasi wao ni nyama, wala si roho.Mwenyezi Mungu atakaponyoosha Mkono wake,yeye anayesaidia atajikwaa,naye anayesaidiwa ataanguka,wote wawili wataangamia pamoja.
6Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.
6Makundi ya ngamia yatajaa katika nchi yako,ngamia vijana wa Midiani na Efa.Nao watu wote wanaotoka Sheba watakuja,wakichukua dhahabu na uvumbana kutangaza sifa za Mwenyezi Mungu.
17Badala ya shaba nitakuletea dhahabu,na fedha badala ya chuma.Badala ya mti nitakuletea shaba,na chuma badala ya mawe.Nitafanya amani kuwa mtawala wako,na haki kuwa mfalme wako.
22Aliye mdogo kwenu atakuwa elfu,mdogo kuliko wote atakuwa taifa lenye nguvu.Mimi ndimi Mwenyezi Mungu;katika wakati wake nitayatimiza haya upesi."