Publicidade

Salmos 12

Kuomba msaada
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi.

1 Mwenyezi Mungu tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;

waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.

2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;

midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

3 Mwenyezi Mungu na akatilie mbali midomo yote ya hila

na kila ulimi uliojaa majivuno,

4 ule unaosema, "Kwa ndimi zetu tutashinda;

midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?"

5 "Kwa sababu wanyonge wanaonewa,

na wahitaji wanalia kwa uchungu,

nitainuka sasa," asema Mwenyezi Mungu.

"Nitawalinda kutokana na wale

wenye nia mbaya juu yao."

6 Maneno ya Mwenyezi Mungu ni safi,

kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,

iliyosafishwa mara saba.

7 Ee Mwenyezi Mungu, utatuweka salama

na kutulinda na kizazi hiki milele.

8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali

wakati yule aliye mbaya sana

ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-